Robo Mwezi. Massimo Longo E Maria Grazia Gullo

Читать онлайн.
Название Robo Mwezi
Автор произведения Massimo Longo E Maria Grazia Gullo
Жанр Зарубежное фэнтези
Серия
Издательство Зарубежное фэнтези
Год выпуска 0
isbn 9788835422280



Скачать книгу

      "Damnabilis ies iom, mirdo cavus mirdo, cessa verunt ies iom, mirdo oblivio ement, mors damnabils ies iom, ospes araneus ies iom…"

      Aliweka kichwa chake kwenye mikono yake ili kutuliza sauti hiyo, lakini haikusaidia. Alipiga magoti na akafunga macho yake...

      "Damnabilis ies iom, mirdo cavus mirdo, cessa verunt ies iom, mirdo oblivio ement, mors damnabils ies iom, ospes araneus ies iom…"

       Sura ya kwanza

       Anaepuka nikijaribu kumkumbatia……….

      "Elio, Elio, njoo hapa! Nisaidie kuanua mboga kabla ya dharuba kuja, tafadhali."

      Elio alikuwa amesimama wima akiwa amevalia viatu vyake vipya na alikuwa akimtazama mamaye, ambaye alikuwa akihangaika katika shughuli zake.

      "Elio! Usisimame tu hapo! Chukua hii!" Alimtikisa na kuweka begi iliyojaa mboga kwenye mikono yake. Elio hakuwa na nia ya kufanya kitu kingine. Alipanda ngazi zilizoko nje ya jengo, akageuka na kufungua mlango. Alianza kutazama taa nyekundu ya lifti ambayo mwangaza wake haivumiliki. Kisha, akaacha kusubiri na kupanda ngazi kwenda kwenye nyumba yake gorofani. Aliweka mboga kwenye meza ya jikoni na kwenda moja kwa moja hadi chumba chake cha kulala kusikiza muziki kitandani.

      Mara tu alipopanda gorofani mamake akaenda kumtafuta. Alisimama mlangoni akipiga kelele: “Unafanya nini? Hatujamaliza bado, njoo unisaidie!".

      "Sawa, nko njiani..." akajibu Elio bila kusonga. Kwa kweli alitaka tu kumwepuka. Giulia akatoka, akitarajia kwamba mara hii itakuwa tofauti. Hakuwa na matumaini. Alikuwa akihangaika kumtia moyo mwanawe, ambaye alikuwa akizidi kuwa mwenye kutojali. Kutoka Mlangoni, aliweza kusikia wazi hatua za dadaye huku akimwita kwa sauti ya furaha. "Elio! Elio! Ondoa makalio kitandani na uje usaidie mama. Anakusubiri huko chini." Alimfokea huku akifahamu kwamba itakuwa bure tu. Elio hakusonga hata inchi moja. Badala yake, aliongeza sauti ya muziki na kuendelea kutazama dari, kana kwamba hakuna kinachotendeka. Giulia, ambaye alikuwa amechoka kutokana na mabishano na mwanawe kuliko kutokana na uchovu, mwishowe alilazimika kupandisha mboga akisaidiana na bintiye, Gaia. Huku akipanda ngazi ya jengo hilo lililo na orofa tano, ambako lifti yaonekana kutofanya kazi kila siku (na kwa kejeli, siku sote haifanyi kazi wakati anapotaka kubeba mboga kupanda ngazi kwenda juu), aliendelea kufikiria kuhusu Elio. Jengo hilo lilipakwa rangi nyeupe na ya machungwa, kama majengo mengine ya baraza la Gialingua, mtaa ambao walikuwa wanaishi. Familia ishirini ziliishi katika mtaa huo, na zilikuwa zimegawanywa katika gorofa ishirini zilizoangalia pande tofauti ya jengo lenyewe.

      "Hii ni mara ya mwisho unafanya hivi!" akamfokea akiwa jikoni. "Tutatatua hii punde to baba yako atakaporejea nyumbani!"

      Elio hakuwa hata anamsikiliza kwa kuwa alikuwa amezama katika muziki huo wa kuchukiza. Hakuna na hakuna anayeweza kutikisa hisia za uchoshi na ubishi aliousheheni. Dunia yake isiyopendeza ilikuwa kama makazi kwake. Huo ndio ulikuwa utu wake na dunia ililazimika kumzoea. Gaia alikuwa tofauti kabisa: alikuwa na umri wa miaka kumi na mitano, ana macho angavu na nywele fupi nyeusi. Saa ishirini na nne hazikotosha kwake kushughulikia maslahi yake yote.

      Giulia alikuwa mwanamke mwenye nguvu pia. Lakini, kinyume cha bintiye, alikuwa na nywele nyeupe zilizopindika, alikuwa mnene kiasi lakini mwepesi na aliyejitolea. Alikuwa mama wa kawaida mwenye umri wa miaka 42: kila wakati alikuwa na ratiba ngumu akijaribu kudumisha usawa kati ya kazi na familia.

      Ilikuwa chakula cha jioni. Hata hivyo, hakuna kelele zilizosikika kutoka chumba cha kulala cha Elio. Kwa kweli, hajasonga tangu alipokimbia kujitosa kitandani na kuvaa vipokea sauti vinavyobanwa kichwani.

      Alisikia sauti ya ufunguo katika kufuli wa mlango wa mbele. Wakati uo huo, huku mlango ukiwa bado haujafungwa vizuri, sauti ya hamaki ya Giulia tayari ilikuwa imemkera mumewe:

      "Hatuwezi kuendelea kufanya hivi!"

      "Mpenzi, wacha niingie chumbani kwanza..."

      Giulia alimbusu mumewe na kurudi kulalamika.

      "Ni kumhusu Elio, sivyo?" alisikika kama aliyekata tamaa wakati alipouliza.

      "Ndio, ni yeye." akajibu Giulia.

      Wakati uo huo, Carlo akatoa mkebe wa chakula ndani ya begi lake ambalo alikuwa akienda kuacha jikoni. Kisha, alikuwa akienda kuweka mkoba wake kwenye kabati la nguo. Ndani ya mkoba huo, kila wakati angeweka jezi ya ziada kwa kwa sababu ya mawimbi ya joto ambayo yalikuwa yakipiga eneo hilo mwezi huo wa Mei.

      Alikuwa mwema, mwenye umri wa miaka arobaini na mbili, mrefu na mwembamba. Nywele zake zilikuwa zimegeuka kijivu, lakini wakati mmoja zilikuwa zinafanana na za bintiye. Uso wake uliochongoka ulikuwa wazi: kwenye pua lake lililofanana na mdomo wa ndege alikuwa akivalia miwani duara ya chuma.

      "Tuizungumzie kumhusu baadaye?" kwa upole alimmwuliza bibiye, akitarajia kwamba atasononeka.

      "Ndio, uko sahihi mpenzi." alijubu, lakini aliendelea kulalamika hadi wakati chakula cha jioni kilipoandaliwa.

      Kwa bahati, Gaia hakuacha kuongea kuhusu siku yake, akichukulia machungu yake madogo kwa njia ya kutia moyo.

      Giulia alikuwa amemaliza kuandaa mezani wakati aliposema:

      "Umwite Elio."

      " Haina maana na unaifahamu." alijibu. "Unajua hatasonga hata inchi moja, isipokuwa aitwe na baba..."

      Giulia, kisha akamgeukia mumewe:

      "Ameshinda katika chumba hicho tangu nilipomrudisha nyumbani kutoka shule. Anazidi kuwa mbaya."

      "Si tulisema atakuwa akirudi nyumbani mwenyewe kuanzia sasa na kuendelea?"

      "Nilikuwa katika eneo hilo...

      Nilikuwa nikinunua mboga..."

      "Kila siku unatoa vizingizio ili kumlinda, lakini tena unalalamika kuhusu tabia yake!"

      Carlo alikuwa akitikisa kichwa chake kama ishara ya kutokubali. Kisha, akaamka kwenye kochi na kwenda kwenye chumba cha watoto.

      Aliingia kwenye chumba hicho cha kulala bila kubisha hodi na kumpata Elio katika mahali papo hapo ambako Giulia alikuwa amemwacha. Alikuwa akitazama dari kwa macho yaliyofunikwa, na alikuwa bado amevalia vipokea sauti vya maskio vyeupe vya Wi-Fi, na hata alikuwa hajavua viatu vyake.

      Carlo hakuamini kwamba alikuwa mvulana yule yule ambaye angeandamana naye kila wakati kwa safari ya kuendesha basikeli. Sasa alikuwa na umri wa miaka kumi na sita, alikuwa mrefu kama yeye, na macho yake ya kijani kibichi bado yalikuwa mazuri, lakini yalionekana yaliyokufa. Katika miaka michache iliyopita, amekuwa akiugua unyongovu. Carlo alikuwa hajasikia kicheko chake kwa muda mrefu, hivi kwamba alikuwa amesahau jinsi inavyosikika. Alikuwa akijuta kwamba hangeweza kukaa naye kwa muda mrefu kama awali. Hata hivyo, alikuwa na shaka kwamba, kufikia sasa, umakinifu wake utathaminiwa.

      Kwa bahati mbaya, miaka kadhaa kabla ya hayo, Carlo alikuwa amepoteza kazi yake kufuatia shida za kifedha. Kufuatia kuongezeka kwa mapato, kampuni hiyo ilihamishwa ngambo, kama kampuni nyingine nyingi.

      Carlo alijitahidi kupata kazi. Hatimaye, akapata kazi katika mji tofauti. Kila siku alilazimika kusafiri muda mrefu na kubadilisha njia ya usafiri mara kadhaa, na kusababisha kuwa mbali na familia yake kwa saa nyingi kila siku. Hurejea nyumbani akiwa amechoka na akili yake kusubaa. Baada ya chakula cha jioni, analala kwenye kochi na bila shaka kuzama kwenye usingizi licha ya jaribio ya kutaka kuwa macho.

      Carlo alidokeza kuwa Elio anapaswa kutoa vipokea sauti vya maskioni. Elio alikubaliana naye tu ili kuepuka kukemewa.

      "Ni wakati wa chakula cha jioni. Njoo ule." Aliamuru. "Mamake alisema kuwa umekaa hapa tangu saa kumi jioni!"

      Elio aliamka kutoka kitandani, na huku akiangalia chini alitembea kupita mbele ya babaye. Na kisha akatembea kuelekea jikoni, bila hata kujaribu kujadiliana na babaye.

      Gaia tayari alikuwa ameketi mezani ambayo alikuwa ameandaa na alikuwa akiwatumia ujumbe rafiki zake na kufanya mipango nao.

      Elio aliketi mbele ya dadaye. Walakini hakuongea neno hata moja naye wakati wote wa chakula cha jioni.

      Chakula cha jioni kilibainika kuwa kisicho cha furaha. Kila mtu alikuwa akiongea